Sunday, 11 January 2015

NISHA'S FILM PRODUCTION KUSAKA KIPAJI KIPYA KWA WANAUME KAZI KWENU

Mwaka mpya mambo mapya,wasanii wapya vipaji vipya navyo tuvipe nafasi au sio?.. Je unahisi una kipaji? Hii ni kwa wanaume kwanza,wanawake nimekuwa nikiwapa kipaumbele sana ila sasa wanaume then tutarudi kwa wanawake.. km una kipaji na umrefu una sifa na muda wa kuigiza what's up picha yako na cv zako.. namaanisha umejuaje km unaweza kuigiza au umefanya kazi ipi na ipi,.. @nishasfilmproduction pekee itavumbua ndoto zako za muda mrefu na utakuwa staring.. ukishirikiana na ma staring wngn kwny filamu ijayo, +255712804050 changamkia tenda au mtag mwny ndoto za kuigiza hapa.. #shukran

Wednesday, 7 January 2015

MANAIK SANGA BAADA YA KUFANYA VIZURI KWENYE HAKUNA MATATA SASA AJA NA ''WAKE UP''

 Manaik Sanga maarufu kama Ze Don aamua kufunga na kufungua mwaka kwa kufanya movie kali inayokwenda kwa jina la ''WAKE UP'' movie hiyo iliyotumia pesa nyingi kuitengeneza inafananishwa na ''EXPANDABLE'' kwani humo kuna mastaa zaidi ya 30 kutoka bongo movie na wengine bongo flevour.
''Natarajia itakuja kufanya vizuri kwani mpaka sasa nimepokea ofa kibao za kuuza filamu hii iliyosheheni mastaa kibao kuna kampuni ya usambazaji filam iliyopo nchini Afrika kusini ya Fojoys inayomilikiwa na Mtanzania ambaye ni muandishi wa habari anayefahamika kwa jina la Fortunatus Kasomfi.'' hayo ni maneno ya Manaik Sanga ''Ze Don''
 Manaik Sanga akiwa na wasanii wenzie location
Wolper,Kajala na Irene uwoya hawa ni baadhi ya mastaa waliopo kwenye movie hiyo ya ''WAKE UP''

Monday, 5 January 2015

NISHA, WASTARA WAWASHUKURU WALE WOTE WALIOFIKA KATIKA DUA ALIYOSOMEWA MAREHEMU SAJUKI

 Msanii Salma Jabu Nisha akiwa na baadhi ya vijana wa Team yake wakipata picha ya pamoja baada ya kumaliza kusoma dua ya Marehemu Sajuki.
 NISHA NA WASTARA WAKIWA NA TEAM ZAO A.K.A TEAM UPENDO
 NISHA NA WASTARA WAKIITIKIA DUA
 NISHA AKIHOJIWA NA WAANDISHI WA HABARI WALIOFIKA KATIKA DUA