Friday, 21 August 2015

Lulu Avamiwa Na Vibaka.

Elizabeth Michael ‘Lulu’ amekumbwa na masaibu mapya ya kuvamiwa na vibaka nyumbani kwake, Mbezi Beach jijini Dar na kumuibia simu zake mbili aina ya Iphone.
Tukio hilo lilitokea hivi karibuni ambapo wezi hao wanadaiwa kuruka ukuta na kufanikiwa kuvunja dirisha la chumba anacholala mrembo huyo na kumliza simu hizo huku yeye akiwa amelala fofofo.
Kwa mujibu wa chanzo makini, wezi hao walitumia mbinu za ‘kisayansi’ kutekeleza zoezi lao kwani siku hiyo Lulu alirudi nyumbani mapema na akawa anachati kwa kutumia moja ya simu hizo, ghafla akapitiwa ambapo alikuja kushtuka na kukuta dirisha limevunjwa na simu zimetoweka.

Gabo: Sijaona Msanii Wa Kushindana Nae Katika Filamu Nchini.

Msanii wa filamu aliyejizolea umaarufu miaka ya hivi karibuni, Salim Ahmed maarufu kwa jina la Gabo amesema haoni msanii anayempa changamato.
Akizungumza kwenye kipindi cha Take One cha Clouds TV, Gabo alisema wengi wamekuwa wakimwambia anaringa kutokana na kuwaambia ukweli.
“Kwa hapa Tanzania sijui ndio maana wanasema mimi naringa,” alisema Gabo alipoulizwa ni msanii gani anayempa changamoto.

Saturday, 8 August 2015

Nisha Azungumzia Mambo Mbalimbali Akiwa China

Star wa filamu nchini Salma Jbau Nisha kwasasa yupo nchini China kikazi na pia kuangalia fursa za kibiashara. Swahiliworldplanet ilipatana nafasi ya kuzungumza nae mchache kama ifuatavyo...