Friday, 28 March 2014

ROSE NDAUKA ADAIWA KUMTIBULIA BATULI DEAL LAKE.


 
Batuli
Mastaa wakubwa wa filamu nchini Yobnesh Yusuph "Batuli" na Rose Ndauka wanadaiwa kuwa kwenye beef chanzo kikidaiwa ni Rose kumtibulia Batuli dili la ile project ya kusafisha jiji iliyofanyika hivi karibuni.
Akizungumza na Ijumaa kwa sharti la kutotajwa jina lake, chanzo kilisema, wazo la project ile alikuwa nalo Batuli lakini Rose akaingilia kati, hali iliyosababisha Batuli amnunie mwenzake.
Alipopigiwa Batuli kwanza aling’aka lakini akasema hapendi kuzungumzia mambo hayo kwani yameshapita huku Rose akieleza kuwa, wazo la project hiyo alikuwa nalo kabla hajajifungua hivyo haoni kama kamtibulia Batuli dili lake.

                                                    Rose Ndauka

WAMACHINGA WAMSUBIRI KWA HAMU ODAMA NA JICHO LANGU.

Filamu mpya ambayo inasubiriwa kwa hamu kubwa kwasasa ni JICHO LANGU toka kampuni ya J-Film 4 Life inayomilikiwa na Odama Jennifer Kyaka. Filamu hiyo inadaiwa ni moto wa kuotea mbali kiasi cha wamachinga kuisubiri kwa hamu kubwa. Odama, Salim Ahmed(Gabo), Thadeo Alexander na Grace Wapunda wameonyesha uwezo mkubwa humo ndani yenye funzo kubwa kwa jamii. JICHO LANGU itaingia sokoni rasmi tarehe 31 mwezi huu wa tatu. usikose kununua nakala yako halisi.

IRENE UWOYA NA JACKLINE WOLPER WAMALIZA TOFAUTI ZAO BAADA YA KUPATANISHWA.

Ule uhasimu uliokuwepo kwa takribani miaka miwili sasa kati ya mastaa wakubwa na warembo Swahiliwood Jackline Wolper na Irene Uwoya hatimaye umefikia tamati baada ya kupatanishwa juzi. Wawili hao walidaiwa kuingia katika beef zito baada ya Uwoya kumsema Wolper vibaya kwenye media ambapo pia aliwahi kukaririwa na gazeti moja akiwa jijini Arusha akisema kuwa Wolper amemroga ili amshushe kwenye sanaa na yeye(Wolper) kuwa juu kisanaa kitu ambacho kilidaiwa kumuudhi sana Wolper.


 Chanzo kimoja kilicho karibu na mastaa hao kikizungumza na Swahiliworldplanet kilisema kuwa aliyewapatanisha ni Steve Nyerere na wote wawili wakakubali kuondoa tofauti zao. "Wolper na Irene Uwoya wameitwa na kupatanishwa na Steve Nyerere sasa wako poa, unajua Wolper alikasirishwa na kitendo cha Uwoya kwenda kwenye media na kumchafua kwa mambo ambayo hakufanya kipindi cha nyuma" kilisema chanzo hicho huku kikikataa kuwekwa jina lake kweupe.

Tungependa kuwapongeza mastaa hawa kwa uamuzi wao mzuri wa kuzika tofauti zao na kuendelea kukuza sanaa ya filamu Tanzania

Monday, 24 March 2014

LULU LOOKS GLAMOROUS IN A NEW PHOTOSHOOT.

Pics from the latest photo shoot of star actress Elizabeth Michael "Lulu" have been released, her styling is hot as she is. Take a look..............





 What do you think ?

PICHA MBALIMBALI ZIKIMUONYESHA MUIGIZAJI SALMA JABU NISHA AKIWA ZANZIBAR.


IRENE UWOYA AMEREMETA KATIKA PICHA MPYA.

Hizo ni picha mpya za star mkubwa wa filamu nchini Irene Uwoya akiwa beautiful kama kawaida


NISHA AJITOLEA KUMSAIDIA MTOTO MWATHIRIKA WA UKIMWI ASIYE NA MBELE WALA NYUMA.

Nisha akiwa na mtoto huyo huko Zanzibar
Star wa filamu nchini Salma Jabu Nisha ameonyesha moyo wa upendo na wa kuigwa katika jamii baada ya kuamua kumsaidia mtoto asiye na wazazi na muathirika wa virusi vya Ukimwi huko Zanzibar ambaye hutengwa na watoto wenzake.

 Kupitia mtandao mmoja wa kijamii Nisha ameandika "Huyu mtoto ndio sababu hasa ilonifanya nikaja huku, yupo darasa la pili,ana miaka 9,baba yake alimkana akiwa tumboni kwa mama yake,mama yake alifariki pindi tu alipomzaa,mtoto huyu mdogo anaishi na virusi vya ukimwi,jamii inayomzuunguka imemtenga,wazazi hawataki watoto wao wacheze nae,shule mwanzo alikataliwa,kula yake Allah anajua,yupo mpweke,SISEMI HIVI KUMTANGAZA LA HASHA, ila ikumbukwe mimi ni msanii na ni kioo cha jamii, jamii inatakiwa ione na kujifunza, inauma sana, ila nipo hapa kwa ajili yake"

Mungu akubariki na kukuzidishia zaidi Nisha kwa kuamua kumsaidia mtoto huyo.

Thursday, 20 March 2014

WASANII WAKUBWA WANAKWAMISHA MAENDELEO YA TASNIA YA FILAMU NCHINI: LIBERTY MSUYA

Liberty
Liberty Msuya aliye muigizaji na producer wa filamu nchini Tanzania huku akiwa na makazi yake nchini Uingereza amefunguka mambo kadhaa kuhusiana na tasnia ya filamu. Star huyo wa filamu za Safari na Laura alifunguka wakati alipoulizwa mambo kuhusiana na usambazaji wa filamu nchini na kushawishi baadhi ya wawekezaji wa kigeni kuja kuwekeza katika sector ya filamu nchini. Liberty pia aliwatuhumu wasanii wakubwa nchini kuwa ndiyo wanakwamisha maendeleo ya kweli katika tasnia kutokana na kuingia mikataba uchwara na wasambazaji amabyo bado inaendelea kuwanyonya na kushindwa kuunganisha nguvu za pamoja na wasanii wenzao wengine ili kutetea maslahi yao.

Kuhusiana na kuwashawishi wawekezaji wa kusambaza filamu toka nje waje Tanzania Liberty alisema Bunge likikubali kuifanya sector ya filamu iwe rasmi ndiyo itakuwa na maana "labda mpaka bunge likubali ndio watu wanaweza kuja kuwekeza katika movies,.nahisi wasanii wakubwa ndio wanatuangusha nilitoa wazo la kuwa na chama cha ma-produser ambacho kipo ila hakina nguvu nikasema tukipe nguvu ili tuwe na wazo moja lengo moja na uamuzi wawote"

"Kama watengezaji movie watengenezaji movies tukisema hatuuzi master tunasema kwa wote kama tamko la watengenezaji movie bongo.then sokoni tushindane kwa kazi mzuri na sio walio na mikataka ndio wanaendelea na kuirudisha chini tasnia badala ya kuipeleka juu bongo movie, huwapromoti watu wao ambao wala sio wasanii wa kweli na kuacha wasanii wa kweli hilo ni latizo sugu"

Wednesday, 19 March 2014

MAPAPARAZI WAZISAKA PICHA ZA ODAMA AKIWA MJAMZITO KWA UDI NA UVUMBA.

Odama
Chanzo cha uhakika kikizungumza na swahiliworldplanet jana kimesema kuwa mapaparazi bado hawajakata tamaa katika kupata picha za star mkubwa anayekimbiza sokoni na movies kibao, Odama Jennifer Kyaka ambaye kwasasa ni mjamzito akitarajiwa kuitwa mama. Wiki iliyopita tuliripoti kuwa mapaparazi wanadaiwa kumshawishi Odama wapate picha zake hata pesa watampa lakini star huyo asiyependa skendo amekataa katakata kwani anaona haina faida kwake zaidi ya kujichafua mbele za jamii.


Sasa chanzo chetu kimetoa habari mpya kuwa Odama bado anasakwa ili apigwe picha huku mapaparazi wakimshawishi mtu mmoja aliye karibu na Odama ampige picha na kuwapa mapaparazi na wao kumpa pesa, lakini chanzo hicho kimekataa pia kwa madai kama mwenyewe hataki hata yeye hataki kufanya hivyo isitoshe shilingi laki 1 wanayotaka kumpa ni ndogo kwani wao wataingiza pesa nyingi wakazipata picha za Odama akiwa mjamzito. "mapaparazi bado wanazitaka picha za Odama wananisumbua kwenye simu kila mara ili nimpige picha halafu niwape wanipe laki moja, siwezi kufanya hivyo hata kwa dawa, hata Odama mwenyewe hayuko tayari, wao wataingiza pesa nyingi kuliko laki moja wanayotaka kunipa" kilisema chanzo hicho.

Ukiachilia mbali chanzo hicho star mmoja wa filamu aliye rafiki wa Odama amesema kuwa Odama kwasasa anaishi kwa machale sana kuogopa kupigwa picha huku muda mwingi akiwa ndani. "Odama yupo kimachale sasa unajua wa...(akiitaja kampuni) wanataka picha zake wanamuwinda wapate picha akiwa mjamzito ila yeye kawachunia"

Ukiachana na habari hizo Odama kwasasa yupo likizo ya uzazi ila filamu yake mpya ya JICHO LANGU kutoka J-Film 4 Life itaingia sokoni tarehe 31 mwezi huu wa tatu, jiandae kununua nakala yako halisi.

Gabo Awaponda Mastaa Wa Filamu Walio Busy Na Skendo Badala Ya Kazi.

Swahiliworldplanet ilipata nafasi ya kuzungumza machache na star wa filamu nchini Salim Ahmed "Gabo Zigamba" kuhusiana na kazi zake za filamu na maisha binafsi hivi juzi kati. Gabo ambaye kipaji chake cha kuigiza hakijifichi huku akiwa tayari amejizolea mashabiki wengi alitiririka kama ifuatavyo katika interview hii ndogo.

SWP: Nani alikushawishi kuingia kwenye sanaa ya uigizaji?

GABO: Ni msukumo wa maisha baada ya plan A na mtazamo wa ndugu jamaa na marafiki

SWP: Umefaidika na nini mpaka sasa tangu uanze kuigiza filamu?

GABO:  Kwa upande wa mafanikio bado naidai sanaa

SWP:  Kitu gani huwa kinakukera zaidi unapokuwa location?

GABO: Kero kubwa ni mijadala ya pre-production ndani production....

SWP: Baadhi ya waigizaji nchini wapo busy kutengeneza skendo ili kuandikwa kwenye media huku kazi zao zikiwa chache na bado haziridhishi je unalizungumziaje hilo?

GABO:  .Ni matumizi mabovu ya akili huwezi kuwa busy na skendo ikiwa huna kaz miliki.....

SWP:  .Umeoa au una mchumba?

GABO:  Nina mke na mtoto mmoja

SWP:  Nini matarajio yako ndani ya miaka 3 ijayo kuanzia sasa?

GABO: Kufanya sanaa kimataifa

Snura Afumwa Kwa Sangoma Akiwa Na Jogoo Na Kufanyiwa Ndumba.

Snura Mushi ambaye ni star wa filamu na muziki nchini amezua habari mpya ya kudaiwa kuwa muumini mzuri wa waganga wa kienyeji a.k.a Sangoma. Kwa mujibu wa Bossngasa blog chanzo kimoja kiliutonya mtandao huo kuwa Snura ana mambo hayo ya kwenda kwa waganga wa kienyeji kila mara.

Baada ya kuzipata habari hizo mtandao huo uliweka mtego kwa Snura na ukanasa baada ya kumuona akiwa amevalia tofauti huku mtu mwingine ikiwa si rahisi kumtambua kuwa ni Snura Star wa wimbo wa Majanga. Snura aliingia kwa mganga huyo akiwa amebeba jogoo jekundu na kufanyiwa ndumba kwa mujibu wa mtandao huo.

                                                 Snura

Saturday, 8 March 2014

HAPPY WOMEN DAY KUTOKA KWA NISHA, JENNIFER WA KANUMBA NA IPTYSAM.

"Hii ni kwa mashabiki zangu wote.. Nisha, Jenifer na Iptysam othman tunawatakia HAPPY WOMEN'S DAY... Tuwapende na kuwaheshimu wanawake.. hakuna kama mwanamke.. mwanamke ndiye anayejua uchungu. Na ndiye mwenye huruma sana kwa jamii.. tunawapenda wanaume ila leo ni women's day" amesema Salma Jabu Nisha


MASTAA 25 WA KIKE TANZANIA WENYE NGUVU KATIKA FILAMU, MUZIKI, UREMBO NA MITINDO.

Leo ni siku ya wanawake duniani ambapo kila pembe ya dunia mwanamke anadhimishwa kwa kutambua mchango wake katika kada mbalimbali. Sekta ya burudani nchini kuanzia filamu muziki, utangazaji, mitindo, urembo na hata blogging imezungukwa na wanawake ambao kwa namna moja au nyingine wametoa power flani katika kazi zao kiasi cha kuzidi kupata mafanikio au kujijengea heshima kwa namna moja au nyingine licha ya kukutana na changamoto kadhaa. Power ni mvuto, power ni ushawishi, power ni hazina ambayo kwa namna moja au nyingine humfanya mtu mwenye nayo kutambulika, kubadilisha au kushawishi vitu au watu flani kubadilika. Swahiliworldplanet imekuletea wanawake 25 kutoka kwenye entertainment industry ya Tanzania wenye power iliyopelekea mabadiliko ya vitu flani au kwa namna yoyote ile. Hawa wanatoka katika filamu, muziki, mitindo, urembo, utangazaji na uandishi wa blogging unaogusa tasnia ya burudani moja kwa moja. kumbuka majina hayajawekwa katika mpangilio maalum kuwa huyu ni wa kwanza na yule ni wa mwisho


1.WEMA SEPETU
 Ni Miss Tanzania 2006 na muigizaji wa filamu nchini, Wema hakauki katika vyombo vya habari nchini kutokana na skendo za mara kwa mara au maisha yake binafsi na ya kimapenzi.


Power quotient: Filamu anayoigiza iwe mbaya au nzuri ni lazima iuze sokoni kutokana na kuwa na nyota ya kupendwa na watu wengi licha ya kuwa kipaji chake cha uigizaji kinatia shaka na wasiwasi.



2. LADY JAYDEE
Ni mwanamuziki wa muda mrefu ambaye nyimbo zake nyingi zimekuwa hits, ana mashabiki wengi na nyimbo zake nyingi hata za zamani hazichuji.


Power quotient: Queen of Bongofleva, Wakati industry ya muziki wa Bongofleva ikionekana kushikiliwa zaidi na wanaume, Jaydee amedhihirisha kuwa kipaji anacho na ni jasiri kuliko mwanaume. Jaydee haogopi mtu yeyote yule anayemuwekea kauzibe mbele yake na kuzuia mafanikio yake. Mpaka sasa hana mpinzani wa kike katika muziki wa Bongofleva licha ya kuwa na zaidi ya miaka kumi kwenye game. She is the most successful "Anaconda" diva in the music industry.


3: FLAVIANA MATATA
Ni mwanamitindo wa kimataifa kutoka Tanzania akiwa na makazi yake nchini marekani, ameshatokea kwenye shows za designers wakubwa duniani na fashion weeks kubwa kama vile London na New York Fashion Weeks. Kupitia foundation yake ya Flaviana Matata anawasaidia wanafunzi mbalimbali wa msingi na secondary hasa wasichana mahitaji mbalimbali ya shule.


Power quotient: Role model wa wanamitindo wengi chipukizi nchini Tanzania na Africa kwa ujumla.


4. YVONNE CHERRYL "MONALISA"
Ni muigizaji wa filamu wa muda mrefu nchini Tanzania, tayari ameigiza filamu nyingi na anakubalika. Filamu yake ya Girlfriend ndiyo inadaiwa kuleta ushawishi na mapinduzi ya kutengeneza filamu za kibiashara nchini.


Power quotient: Endless Fame and talent, ni zaidi ya miaka 12 tangu Monalisa aanze kuigiza na kupata umaarufu na hawajawahi kuchuja tofauti na waigizaji wenzake wengi wa kike aliowika nao miaka hiyo ambao hawajulikani walipo huku wengine wakijikongoja kwenye tasnia. Monalisa pia anachukuliwa kama atress wa Tanzania mwenye sifa za kuwika kimataifa.


5.SALAMA JABIRI
Ni mtangazaji wa muda mrefu sasa alipijipatia umaarufu na na kipindi cha Planet Bongo na sasa Mkasi show vyote vikirushwa EATV.


Power quotient: Game changer...ingawa kwa sasa Salama hatangazi tena kipindi cha Planet Bongo lakini aliweza kuleta mapinduzi kwa wanamuziki wengi wa Bongofleva kufanya video nzuri kutokana na kuzikosoa video mbovumbovu bila kumuonea aibu mtu so wanamuziki wengi wakawa na hofu ya kufanya video zisizo na viwango kwa kuogopa kulipuliwa na salama. mapaka leo watu wanakumbuka mchango na nguvu ya bidada huyu.


6.RITA PAUSLEN(MADAM RITA)
Ni mwanzilishi wa shindando maarufu la kusaka vipaji nchini liitwalo Bongo Star Search aliyeibua vijana wengi kupitia shindano hilo.


Power quotient: Madam Rita ni kimbilio la vijana wengi wanaotaka kutoka kupitia muziki na kiuchumi lakini hawajui waanzie wapi so wanajitosa Bongo Star Search. Akiwa kama mwanamke ameweza kilisimamia shindano hilo na kusimama vizuri tangu lianzishwe mpaka leo licha ya washindi wengi kushindwa kufurukuta baada ya kushinda.


7.MARIA SARUNGI -TSEHAI
Ni mwandaaji wa mashindano ya Miss universe, Miss Eath Tanzania ambaye ameibua vipaji vingi vya urembo kupitia mashindano anayoandaa.


Power quotient: Ameweza kuondoa kasumba kuwa warembo wa Tanzania hawafurukuti katika mashindano ya kimataifa kutokana na warembo wengi wanaoshinda katika mashindano anayoyaandaa kufanya vizuri kimataifa kuliko mwandaaji mwingine yeyote wa mashindano ya urembo nchini. Mfano. mzuri ni Flaviana Matata, Miriam Odemba na Tetemaria Mallya ambao waliingia final za mashindano ya kimataifa na kushika nafasi za juu.
Soma list nzima katika link hii hapa 25 Powerful Women In the Tanzanian entertainment industry.

Friday, 7 March 2014

Masai Nyotambovu Kuutambulisha Wimbo Wake Mpya Leo Hii Friday Night Live, Rich Mavocko Na Kitokololo Nao Ndani.

Hatimaye ile video ya wimbo mpya ya mchekeshaji Masai Nyotambovu aliyomshirikisha Rich Mavocko na Kitokololo anaitambulisha rasmi leo saa tano usiku katika kipindi cha Friday Night Live kinachorushwa EATV. Hivyo mashabiki wa Masai Nyotambovu msikose kutazama kipindi hicho, sapoti yenu ni muhimu sana.


Wednesday, 5 March 2014

NISHA, KING MAJUTO, WASTARA NA HEMEDY WAIFANYA GUMZO KUUZA SANA SOKONI.

Filamu ya Gumzo iliyoingia sokoni hivi karibuni kutoa Nisha's Film Production inadaiwa kufanya vizuri sokoni katika nchi mbalimbali za Africa mashariki na kati. Vile vile kupitia mtandao mmoja wa kijamii Nisha amendika "Habari Tanzania na dunia kwa ujumla.. siku zote naamini asoshukuru si muungwana,mm naomba nichukue fursa hii niwashukuru sana kwa mapokezi ya filamu ya NISHA'S FILM PRODUCTION.. filamu ya ‪#‎GUMZO‬ kiukweli hadi sasa idadi ya mauzo yanayotokea siachi kusema ahsante Mungu.. na nyinyi mashabiki zangu,maana naamini ninyi ndio muliyoyafanya maajabu haya.. nawapenda sana.. na kwa wasionunua #GUMZO hujachelewa,ipo madukani pata nakala yako sasa... humu hamna watoto ila nawashukuru sana maana wao ndio wamevunja record"

Filamu ya Gumzo imewakutanisha mastaa wakubwa kama Nisha, King Majuto, Wastara na Hemedy. Hakikisha unapata nakala yako halisi kama bado hujaiona Gumzo.